Fredy Swai, ni msanii mpya wa Bongo Movie ambaye ametambulishwa rasmi kama Mrithi wa hayati Steven Charles Kanumba, msanii maarufu wa Bongo Movie ambaye alifariki ghafla miaka kadhaa iliyopita jijini Dar. Mama mzazi wa marehemu Kanumba, Bi. Flora Mtegoha, ndiye aliyempitisha kijana huyo kuitwa Mrithi wa Kanumba baada ya kumuona ana mengi anayofanana na marehemu mwanae, ikiwemo sura. Katika Exclusive Interview ya Global TV, amefunguka mengi kuhusu wasifa wake huo.