Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema kuna kasumba ya Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kutoa kipaumbele kwa wawekezaji wanje na kuweka urasimu mwingi kwa wawekezaji wandani.
Samia ameyasema hayo Mkoani Pwani wakati akizindua kiwanda cha Raddy Fiber ambacho ni cha nne kwa ukubwa Afrika kwa sasa lakini kitakapo kamilika ujenzi wake kitakuwa cha tatu Afrika.
Rais Samia amesema kuchelewesha uwekezaji nchini ni kuchelewesha ajira kwa watu ambao wangeajiriwa katika viwanda husika pia uchelewesha mapato ya kodi ambayo Serikali inapata kwa viwanda.